This archive report was first published on 17 July 2019.
Gavana wa Machakos Alfred Mutua alimtembelea Raila Odinga katika afisi yake ya Capitol Hill mnamo Jumatano, Julai 17, 2019, wakifanya mazungumzo kuhusu mambo kadhaa ikiwemo siasa za uchaguzi mkuu 2022.
Alfred Mutua, ambaye tayari ametangaza azma yake ya kuwania urais 2022, alifichua kwamba alimuomba Raila ushauri wa jinsi anaweza jizolea kura na pia iwapo angeshirikiana naye kuunda chama cha kisiasa.
Wawili hao walikubaliana kushirikiana ili kupigana na ufisadi na kuhakikisha kwamba viongozi wote ambao watahusishwa na donda ndugu hilo wanaadhibiwa vilivyo.
Alfred Mutua alisema kwamba walikubaliana na Raila nchi inahitaji kiongozi wa kuleta maendeleo ambaye anaweza pigana na ufisadi kwa ujasiri.
Wawili hao walikubaliana kuendelea kujadiliana mara kwa mara kuhusu mambo muhimu ambayo yanaathiri taifa.
Source: Tuko.co.ke