This archive report was first published on 17 July 2019.
Polisi wa Kaunti ya Murang'a wamenasa noti za alfu moja kwenye kitita cha shilingi laki tisa na tisa. Hii ni kufuatia kujaribu kwa watu watatu kufanya kazi ya ghushi kwa kiasi kikubwa.
Watu hao watatu walikamatwa katika eneo bunge la Kandara. Mmoja wa washukiwa hao, Stephen Murigi, alikuwa ametakiwa kufika kwenye kituo cha polisi cha Kabati ambapo anachunguzwa kwenye kesi tofauti.
Maafisa wa polisi waligundua alikuwa na fedha hizo kwenye gari lake na hivyo kumtia mbaroni. Kamanda wa polisi wa Murang'a, Joseph Kinyua, alisema hili.
Polisi pia walipata kifaa ambacho hutumika kutengeneza fedha hizo ghusi, kwa kuwa kifaa hiki kilikuwa kwenye gari la Stephen Murigi.
Washukiwa wengine wawili, Joyce Muthoni na Raphael Njoroge, walikamatwa katika eneo la Kaburugi wadi ya Ng'araria baada ya kujaribu kuweka shilingi alfu 17 kupitia kwa mhudumu wa M-Pesa. Mhudumu huyo aligundua na hivyo akawahadaa wasubiri kabla ya yeye kujulisha wananchi na hivyo gari la wawili hao likazuiliwa na wananchi kabla ya kuwakamata na kuwapeleka hadi kwa maafisa wa polisi.