This archive report was first published on 15 July 2019.
Kitendo cha mwizi huyo kilitokea katika kanisa la Pentecostal Evangelistic Fellowship of Africa (PEFA) katika kaunti ya Nyandarua, Kenya.
Wenyeji wa kijiji cha Engineer walisema kisa hicho kilitokea Jumatatu, Julai 15, 2019.
Alama ya mwizi huyo ilikuwa kinywa wazi, kwani alikuwa amejitolea kufanya maombi ya msamaha.
Barua ya mwizihuyo ilisema alijutia kwa nini akavunja na kuingia kanisani huku akitarajia kupata sadaka ndani, lakini akatoka mikopo mitupu.
Alisema mshirika mmoja alikuwa amempa ripoti kuwa kulikuwa na kitita che fedha humo ndani.
“Nilikuwa nimetumwa hapa kanisani na mmoja wa washirika akiniambia kuna pesa zimewekwa humu. Lakini sikupata chochote. Mungu awabariki nyote na mniombee. Asanteni,” barua hiyo ilisema.
Alisema mshirika mmoja alikuwa amempa ripoti kuwa kulikuwa na kitita che fedha humo ndani.
Kitendo cha mwizi huyo kilidhibitishwa na mhubiri Peter Wanyoike aliyesema mwizi huyo aliingia katika kanisa hilo baada ya kukata mabati.
Alisema washirika wake walikubali msamaha wa mwizi huyo lakini bado wakaripoti kisa hicho.
“Tulipata barua kanisani wakati ambapo maafisa wa polisi walifika na kuanzisha uchunguzi wao. Mwizi huyo alikuwa ameamini kuna fedha kanisani, lakini tumemsamehea na kuanza kumuombea aokoke. Tunamuomba aje atubu na aokoke,” Wanyoike alisema.