This archive report was first published on 10 July 2019.
Mombasa: Mamba Hataki Kukaa Madimbwi Yao, Wakimbia Kwa Matajiri Nyali ¶
Wakazi wa Nyali, Mombasa, wamekuwa wakilalamika kuhusu mamba ambao wamekataa kukaa katika madimbwi yao na kuhamia makazi ya matajiri.
Wanyama hao wamekuwa wakipiga kambi mitaani na kuwasumbua kilasiku huku wakiwafanya kuishi kwa uoga mwingi.
Wakazi wa eneo hilo wanasema wanyama hao wamekuwa wakirandaranda ovyo mtaani hapo kwa wiki mbili sasa.
Maafisa wa Shirika la Wanyama Pori (KWS) waliitwa na kuwaregesha wanyama waliokuwa wameonekana eneo hilo lakini walirejea baadaye na kuendelea kurandaranda mitaani.
Ali Safari, meneja wa hifadhi hiyo alisema wanakarabati madimbwi ya wanyama hao ili kuzuia mamba hao kutoroka.
Eneo la Mamba Village ambalo lipo mkabala na Nyali, linasemkana kuwa eneo kubwa zaidi la kufugia mamba eneo hili la Saharan barani Africa na linadaiwa kuwa na zaidi ya mamba 10,000.
Wakazi wa Nyali wanasema wanyama hao huenda walitoroka madimbwi yao katika eneo la Mamba Village, linalomilikiwa na aliyekuwa mbunge wa Nyali Bw. Hezron Awiti.
Wanadai wanyama hao sasa wamekuwa wakipiga kambi mitaani na kuwasumbua kilasiku huku wakiwafanya kuishi kwa uoga mwingi.
Wakazi wa Nyali jijini Mombasa wamekuwa wakilalamika kuhusu mamba ambao wamekataa kukaa katika madimbwi yao na kuhamia makazi ya matajiri.