This archive report was first published on 9 July 2019.
Mbunge wa Njoro, Charity Kathambi, alizindua miradi ya maendeleo katika Shule ya Sekondari ya Mauche Samoei na Shule ya Msingi ya Lulukwet, Wadi ya Mauche, Jumatatu, Julai 8, 2019.
Alivalia sare ya shule na kuzindua mradi huo, akionekana akiwasemeza wanafunzi na kuwafahamisha umuhimu wa elimu.
Alisema kuwa, ili kupatikana elimu bora, ni lazima mazingira na miundo mbinu zinazofaa kuwekwa.
“Madarasa niliyozindua katika Shule ya Sekondari ya Mauche Samoei na Shule ya Msingi ya Lulukwet, Wadi ya Mauche mchana wa leo yatasaidia kupatikana elimu bora, kuchochea masomo na kuhakikisha alama bora,” alisema.
Naunga mkono Mtaala mpya wa CBC ndio maana nahimiza kila jamii na wadau katika sekta ya elimu kukaa chini na kuafikiana kuhusu mfumo bora utakaosaidia mwanafunzi kutumia uwezo wake wote, kupata mtakabali unaofaa…ukaokwenda na mahitaji ya viwanda,” alisema.
Alitangamana huru na wanafunzi baada ya uzinduzi huo, akionekana akiwasemeza baadhi yao na kuwafahamisha umuhimu wa elimu.
Alivalia sare ya shule na kuzindua mradi huo, akionekana akiwasemeza wanafunzi na kuwafahamisha umuhimu wa elimu.