Skip to main content

Ujauzito na Uzazi: Kuvuja Damu Haiwezi Kuwa Dalili Nzuri

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 2 January 2022.

Ujauzito ni mchakato changamano ambao unaweza kuwa na matatizo mbalimbali. Kuvuja damu wakati wa ujauzito katu si dalili nzuri, na hii ni kwa sababu mzunguko wa kihomoni kila mwezi umekatizwa.

Ukuta wa uterasi ambao huambuka kila mwezi wakati wa hedhi sasa unatumika kumkuza mtoto aliye tumboni. Hata hivyo, unaweza kuvuja damu wakati wa ujauzito, wakati ambapo mimba inajitundika kwenye ukuta wa uterasi.

Damu hii hutoka wiki za awali za ujauzito na kwa kawaida haitoki kwa wingi. Aidha, unaweza kuvuja damu kutokana na mwasho kwenye lango la uzazi, au ikiwa kuna maambukizi, au ikiwa mimba imejitundika nje ya uterasi (ectopic pregnancy), au ikiwa kuna hatari ya mimba kutoka.

Matatizo haya huhitaji kuangaliwa na mwanajinakolojia. Aidha, huenda uchunguzi wa maabara ukahitajika na wakati mwingine kupigwa picha ya sehemu ya nyonga.

Ujauzito ni mchakato changamano ambao unaweza kuwa na matatizo mbalimbali. Kuvuja damu wakati wa ujauzito katu si dalili nzuri, na hii ni kwa sababu mzunguko wa kihomoni kila mwezi umekatizwa.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →