This archive report was first published on 12 November 2021.
Uingereza imeahidi kushirikiana na Kenya kupiga vita ufisadi na kufufua mifumo ya uchumi baada ya athari za Covid-19.
Wakati wa kuhutubia vyombo vya habari jana, Mbunge wa Uingereza anayesimamia Biashara ya Kenya, Theo Clarke, alisema Uingereza imejitolea kushirikiana na Kenya kupiga vita ufisadi.
Alipongeza pia Kenya kwa juhudi zake za kukabiliana na athari hasi za mabadiliko ya hali ya anga, akirejelea Kongamano la Kitaifa la COP26.
“Serikali ya Kenya imejitolea kushirikiana na Kenya kukomesha ufisadi hasa kuambatana na ripoti iliyotolewa na Tume ya Kitaifa kuhusu Maadili na Kukabiliana na Ufisadi Kenya (EACC) mnamo 2015,” alisema Bi Clarke.