Skip to main content

Mama Akataa Kupeana Zawadi Kwa Maharusi, Akirejea Nyumbani Kwa Njaa

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 1 November 2021.

Na Leah Makena, Keroka, Kisii

Mama wa hapa alishangaza wengi alipokataa kupeana zawadi kwa maharusi na kurejea nyumbani kwa kukosa chakula sherehe ya harusi.

Alipokuwa jirani ya binti aliyekuwa na harusi, mama alikuwa akihudhuria mikutano ya harambee na kuchangia pakubwa kufanikisha harusi hiyo kando na kununua zawadi ya sufuria mbili alizobeba ili kukabidhi wanandoa.

Sherehe iliendelea ilivyotarajiwa hadi jioni, wakati waliohudhuria walipoagizwa kujipanga ili wapate chakula.

Alipokataa kufuata utaratibu na kujiunga na upande wa wazazi, mama alisema kwamba alikuwa mtu wa maana kwa kidosho.

“Tulikuwa tumeonyeshwa wazazi wa pande zote mbili na hao pekee ndio wanatumia meza spesheli. Hao wengine wanapewa chakula kutoka upande wa pili. Hatutaki msongamano upande huu kwa sababu ni muhimu kuheshimu wazazi wa maharusi,” mmoja wa wapishi alieleza.

Alipoulizwa kuhusu hali hiyo, mama alisema, “Kwa nini nitoe zawadi na nimebaki nikiwa njaa pekee yangu? Sasa nimepata matokeo ya kujishughulisha kwa muda mrefu kwani hata niliowashughulikia leo hawanitambui. Nitatumia sufuria kupikia kwangu, hata sikuwa na za kutosha jikoni.”

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →