This archive report was first published on 4 July 2019.
Seneta wa Elgeyo Marakwet, Kipchumba Murkomen, amekabiliwa na vikwazo vya kijamii baada ya kudai kwamba maafisa wa polisi walikosea kumkamata mkurugenzi mkuu wa mawasiliano ya kidijitali katika ikulu, Dennis Itumbi, kwa kueneza barua ghushi inayodaiwa kuwa na ujumbe wa kumuua Naibu Rais William Ruto.
Itumbi alikamatwa Jumatano Julai 3, na maafisa kutoka Idara ya Upelelezi DCI kwa kuhusishwa na barua ghushi hiyo.
Murkomen alitaka maafisa wa upelelezi kuwakamata waliohusika na barua hiyo, lakini sio mtu yeyote tu.
Alisema, "Kwa hivyo, itumbi alikatwa kwa kueneza barua ghushi kwenye kundi la WhatsApp la wanachama wa Tangatanga, ni watu wangapi wamesambaza barua hiyo?, hebu na vyombo vyote vya habari vilivyoeneza barua hiyo pia vichukuliwe hatua," Murkomen alisema kwenye mtandao wa Twitter.
Itumbi alifunguliwa mahakamani Alhamisi Julai 4, na atazuiliwa tena kwa siku tano ili uchunguzi zaidi ufanywe dhidi yake.