Skip to main content

Peter Munya: Waziri wa Kilimo atawapa Mafunzo ya Uvumilivu kwa Vijana 2,000

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 26 August 2020.

Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Peter Munya amesema kuwa sekta ya uvuvi ya nchini itakuwa na uwezo wa kuajiri mamia ya vijana wakati wa kuimarishwa.

Alisema hii wakati alipozuru kituo cha Liwatoni, ambacho ni maalum kwa kuimarisha sekta ya uvuvi na kilichogharimu serikali Sh318 milioni kukirekebisha.

Waziri Munya alisema kuwa wizara yake imeanza kuwalinda wavuvi na kuimarisha sekta hiyo ili kufufua uchumi wa taifa.

Alisema asilimia 30 ya samaki itakayovuliwa baharini itauzwa kwa bei ya reja reja huku 70 ikisafirishwa kuuzwa nchi za kigeni.

“Liwatoni itabadilisha na kuimarisha sekta ya uvuvi nchini na hivi karibuni kituo hiki kitaanza kazi ambapo mashua za uvuvi zitatia nanga eneo hili kuleta samaki. Itakuwa na uwezo wa kuweka tani 250 za samaki lakini tunapania kupanua ili kufikia tani 500,” alisema Bw Munya.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →