Skip to main content

Waziri wa Zamani John Cheruiyot Ahukumiwa Miezi Mitatu Gerezani

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 19 July 2020.

Waziri wa zamani wa Maendeleo, John Cheruiyot, alihukumiwa miezi mitatu gerezani siku ya Jumanne, Julai 14, kwa kushindwa kulipa deni ya KSh2.3 milioni.

Cheruiyot, ambaye alihudumu chini ya serikali ya hayati Rais Daniel Moi, alipelekwa katika Gereza la Viwandani kutumikia kifungo chake.

Alishtakiwa kwa kukataa kumlipa Lango Odhiambo pesa za kuchapisha makaratasi 50,000 za Chama cha KANU mwaka 1994.

Cheruiyot alishtakiwa pamoja na wanachama wengine wa zamani wa KANU, Joseph Kamotho, Wilson Ndolo, na Japheth Lijoodi, ambao wote ni marehemu.

Alishindwa kutimiza ahadi ya kulipa pesa za kuchapisha makaratasi ya KANU baada ya kutoa hunda la KSh50,000 na kufuatiliza hunda la KSh10,000, ambalo lilikataliwa na baadaye kushindwa kulipa deni lililokuwa limesalia la KSh565,000, ambalo liliongezeka hadi KSh1.6 milioni.

Cheruiyot alikuwa amehukumiwa miezi sita gerezani mnamo 2015, lakini aliachiliwa huru kwa dhamana baada ya kuingia kwenye mwafaka wa kulipa pesa hizo polepole.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →