Skip to main content

Wageni katika sherehe ya mtoto wa Citizen TV wanasa Covid-19

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 18 July 2020.

Wageni katika sherehe ya mtoto wa Citizen TV wanasa Covid-19

Sherehe ya kuzaliwa kwa mtoto wa Stephen Letoo, mwanahabari wa Citizen TV, ilikuwa na matokeo mabaya baada ya wageni wengi kuambukizwa na virusi vya COVID-19.

Chanzo chetu kilisema idadi ya waliohudhuria sherehe hiyo ilikuwa kubwa zaidi ya idadi ya watu 15 wanaoruhusiwa na serikali.

Sherehe ilifanyika usiku kuchwa katika nyumba ya Stephen Letoo na hivyo walivunja sheria za kifungu cha kisiasa.

Moja wa waliohudhuria alikuwa na dalili za COVID-19 na baada ya kupimwa alipatikana na virusi vya ugonjwa huo.

Letoo alikuwa mtu wa pili kukutwa na virusi hivyo baada ya vipimo alipata majibu yaliyosema tayari alikuwa na virusi vya corona.

Imebainika kuwa baadhi ya waliokuwa kwenye sherehe tayari walisafiri na kurejea mikoani.

Chanzo chetu kilisema, "Kuna walioondoka Nairobi, mmoja kutoka Kilgoris na mwingine Narok. Inasikitisha kwa kuwa wanatangamana na watu ingawa waetakiwa kijitenga,"

Watu walikuwa 20 na ilifaa wawe 15 na kwa kuwa waliokuwa wakija na kutoka wakati wa sherehe.

Sherehe iliendelea usiku hadi Jumapili, Julai 12 wakati baadhi ya wageni walipoondoka kwenda makwao.

Letoo yupo nyumbani kwake akijitengea huko, huku baadhi ya waliopata matokeo ya vipimo na kukutwa wana virusi wakijitenga pia.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →