Skip to main content

Wavulana 2 wa miaka 6 wauguza majeraha baada ya kushambuliwa kwa kisu

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 9 July 2020.

Wavulana wawili wa miaka 6 wameguza majeraha mabaya baada ya kushambuliwa na jamaa mmoja aliyewakashifu kwa kumuibia mahindi katika kijiji cha Kiptere.

Chifu wa kata ndogo ya Kiptere David Kipkurui amethibitisha kisa hicho na amesema jamaa huyo atachukuliwa hatua za kisheria.

Aliposhambulia watoto hao, jamaa huyo alikuwa na kisu na alikuwa akidai kuwa ni njia moja ya kuwaadhibu.

Wakazi wa eneo hilo waliosikia nduru walipata watoto hao wakiwa wamelala sakafuni huku damu ikitiririka.

Alipotekeleza kitendo hicho cha unyama, mshukiwa alijaribu kutoroka lakini alikamatwa na wakazi waliompeleka katika kituo cha polisi cha Sondu ambapo anazuiliwa kwa sasa.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →