This archive report was first published on 9 July 2020.
Gavana wa Mombasa Hassan Joho na mbunge wa Suna Mashariki Junet Mohammed wamefunga safari hadi Dubai kumuona Raila Odinga, ambaye amekuwa nchini Dubai baada ya kufanyiwa upasuaji katika hospitali moja ya kijerumani.
Wawili hao ni wafuasi wakubwa wa Baba na kisiasa wamejipa jina la 'Baba Boys', na wamekuwa wakirindima siasa zake na chama chake cha chungwa.
Julai 9, 2020, Joho alitangaza kuhusu safari yao kumjulia hali ya Baba kupitia ukurasa wake wa Twitter.
Wakati wa kuongezeka kwa maoni kuhusu safari yao, Raila alikuwa amelazwa kwenye hospitali moja ya Ujerumani nchini Dubai ambapo familia ilisema alifanyiwa upasuaji huo.
Junet Mohammed na Joho ni baadhi ya wafuasi sugu wa Baba na wamekuwa wakirindima siasa zake na chama chake cha chungwa.
Junet alizua mjadala baada ya kusema wao humfuata Raila kama ng'ombe na hivyo hawawezi kuenda kinyume na atakalo.