This archive report was first published on 6 July 2020.
Rais Uhuru Kenyatta amesema kufyu kwa virusi vya corona kwa siku 30 zijazo itaendelea kawaida. Alisema hii wakati wa kujibu maswali kuhusu mikakati iliyopo ya kukabiliana na maradhi ya Covid-19.
Alisema kila mtu anapaswa kuwa na tahadhari kubwa na kuzingatia maelekezo ya Wizara ya Afya kuhusu kuzuia kusambaa kwa virusi vya ugonjwa huo.
Aliongeza kwamba magari ya uchukuzi wa umma yatakuwa na uwezo wa kuingia na kutoka katika maeneo yaliyokuwa yamefungwa awali lakini kwa vibali maalum.
Alisema pia kwamba safari za ndege za ndani zitakuwa na uwezo wa kufanya kazi kuanzia Julai 15 huku safari za ndege za kutoka na kuingia nchini zikiruhusiwa kuanzia Agosti 1.
Alisema hakuna mikutano ya hadhara itakayoruhusiwa kwa siku 30 zijazo na maeneo ya kuabudia kufunguliwa kwa awamu na madrissa pamoja na shule za masomo ya dini kwa vijana makanisani kubakia ilivyokuwa awali.
Aliongeza kwamba uchunguzi kuanzishwa kuhusiana na visa vingi vinavyoripotiwa vya dhulma za kijinsia, dhulma dhidi ya haki za watoto na visa vingi vya mimba za mapema miongoni mwa vijana ambao bado wanasoma katika shule za msingi na sekondari.