This archive report was first published on 2 July 2020.
Korti yaamuru Raila na Uhuru kurekodi taarifa kuhusu kesi ya CCTV ¶
Maafisa wawili wa usalama walishtakiwa kwa kufuja video ya CCTV ya Rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa ODM, Raila Odinga wakikagua miradi ya serikali usiku wa Juni 2, 2020.
Maagizo hayo yaliwaagizwa na mahakama moja jijini Nairobi ambapo wafanyakazi wawili wa Hoteli ya Stanley Hotel walishtakiwa kwa kufuja video ya CCTV ya wawili hao.
Maafisa wawili wa usalama walishtakiwa na makosa ya kutoa taarifa kinyume na sehemu ya 17(1) ya matumizi mabaya ya tarakili na uhalifu wa mtandaoni.
Walikuwa wakitumia gari ndogo ambapo walichomoka na kuanza kukagua mradi wa kurembesha eneo la Kenyatta Avenue.
Video hiyo ilionyesha Rais Uhuru ndiye alikuwa akiendesha gari hilo na alikuwa wa kwanza kutoka kabla ya Raila kumfuata.
Wakili wa wawili hao, Danstan Omari, alihoji kwamba makosa dhidi ya wawili hao hayapo kwenye sheria.
"Mashtaka haya ya kuchapisha taarifa ya CCTV hayapo kwenye sheria. Wateja wetu hawakuwa Ikulu na hawajawahifika katika shirika lolote la serikali na kutoa kanda ya CCTV ya serikali," alisema Omari.