This archive report was first published on 30 June 2020.
Polisi wa Makueni walinasa basi lililokuwa limebeba abiria 24 walioripotiwa kusafiri kutoka Mombasa kufikia siku ya 30 Juni 2020.
Abiria hao walikuwa wanelekea maeneo tofauti, na kufanya polisi kuwa na wasiwasi kwamba walikuwa wakisafirisha watu kutoka Taita Taveta.
Kamishna wa Makueni Maalim Mohammed aliiambia kuwa abiria hao walipelekwa hadi Chuo cha Mafunzo ya Uuguzi cha Makindu ambapo waliwekwa karantini ya lazima.
Alisema, "Marufuku ya kutoka na kuingia Nairobi na Mombasa ingalipo. Walituhadaa kuwa walikuwa wakisafirisha watu kutoka Taita Taveta lakini tuliwanasa,".
Alisema wasafiri hao walipelekwa hadi Chuo cha Mafunzo ya Uuguzi cha Makindu ambapo waliwekwa karantini ya lazima.
Abiria hao walishikilia kwamba hawakusafiri kutoka Mombasa bali waliabiri basi hilo katika kituo cha mabasi cha Wote.
Idadi kubwa ya wagonjwa wa coronavirus wamekuwa wahudumu wa hoteli zilizoko barabara kuu ya Mombasa-Nairobi.