Skip to main content

Watu 64 wanaswa wakijaribu kuvuka kizuizi cha Blue Post Thika

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 25 June 2020.

Polisi wamewakamata watu 64 wanaodaiwa walijaribu kuwahonga polisi wanaoshika doria katika kizuizi cha Blue Post mjini Thika, kaunti ya Kiambu.

Watu hawa walikuwa wakijaribu kuvuka kizuizi hicho ili kuingia kaunti ya Murang'a, lakini walikamatwa na polisi.

Waliokamatwa ni madereva 16 na abiria 48 waliosafiri kutoka Nairobi.

Maafisa wa polisi waliosemekana kuwasaidia wasafiri walionywa huku adhabu kali ikitangazwa kutolewa watakaonaswa wakivunja sheria.

Maagizo ya kuingia na kutoka jijini Nairobi na viunga vyake yilitangazwa na Rais Uhuru Kenyatta kutokana na kuongezeka kwa visa vya maambukizi ya coronavirus nchini.

Waziri wa Afya Mutahi Kagwe alitangaza kuwa baadhi ya watu wanapuuza maagizo hayo na kutumia njia mbadala kupenyeza nje na ndani ya jiji la Nairobi.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →