Skip to main content

Idadi ya walioambukizwa virusi vya corona nchini Kenya yavuka 5,000

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 24 June 2020.

Idadi ya walioambukizwa virusi vya corona nchini Kenya iliongezeka hadi 5,206 kufikia Jumatano, Juni 24, 2020, baada ya wagonjwa wengine 245 kuthibitishwa kuugua maradhi hayo.

Wizara ya Afya ilipimwa sampuli 4,895, ambazo zilichunguza kuwa zinaambukizwa virusi vya corona.

Wakati uo huo, Katibu wa Afya Dkt. Mercy Mwangangi alisema kuwa idadi ya sampuli zilizochunguzwa nchini Kenya iliongezeka hadi 151,396 tangu Machi 13, 2020, wakati kisa cha kwanza kiliripotiwa nchini.

Alisema pia kuwa idadi ya waliopona kutoka kwa virusi vya corona iliongezeka hadi 1,823, huku idadi ya waliofariki nayo iliongezeka hadi 128 baada ya watu wengine wawili kufariki dunia kutokana na maradhi hayo hatari.

Alisema pia kuwa kuna hatari kubwa zaidi ya kuambukizwa virusi vya corona mtu akiwa mjini Mombasa kuliko akiwa mjini Nairobi.

Idadi ya visa vya maambukizi ya virusi vya corona kote ulimwenguni ilikuwa 9.38 milioni kufikia Jumatano, Juni 24, 2020, ikiwemo wagonjwa 5,073,233 waliopatanafuu na 480,444 wakiaga dunia.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →