This archive report was first published on 22 June 2020.
Mkutano wa Jubilee KICC ulikuwa na maana kubwa kwa sasa kwa sababu ulikuwa na wajumbe wengi wa chama hicho, ikijumuisha Rais Uhuru Kenyatta na Naibu wake William Ruto.
Walipokuwa wakiagana, Rais Uhuru na Naibu wake walionekana wakisema mzaha na hata kukaa kama waliokuwa wakitupiana mzaha wa iana fulani.
Picha hii ilikuwa na maana kubwa kwa wafuasi wa Rais Uhuru na Naibu wake kwa sababu ilionyesha urafiki wao kisiasa kama ulivyokuwa.
Hata hivyo, sasa inaonekana kuwa urafiki huo umefifia baada ya mkutano huo.
Wandani wa Naibu wa Rais William Ruto wamekuwa wakitimuliwa kutoka nyadhifa za bunge tangu ripoti za kufifia kwa urafiki wa Uhuru na Ruto.
Aden Duale alitimuliwa Jumatatu, Juni 22 kutoka wadhifa wa kiongozi wa wengi, na hii inaonyesha kuwa urafiki kati ya Rais Uhuru na Naibu wake umefifia.