This archive report was first published on 21 June 2020.
Mwimbaji maarufu Akothee amesema yuko tayari kuolewa na miaka 40, baada ya kueleza umuhimu wa kuwa na mwenzake wa kumsaidia katika ufanisi na kutafuta ushauri kutoka kwake.
Alisema hili katika ujumbe mrefu kwenye Instagram, ambapo alimsifu Gavana wa Nairobi Mike Sonko na mke wake Primrose walipokuwa wakisherehekea miaka 21 katika ndoa.
Akothee aliongeza kuwa vijana wengi hawatambuia kuwalea watoto katika uhusiano uliovunjika hawajaui maisha ya faraghani yanavyoambatanishwa na majonzi na masumbuko.
Alisema kuwa sasa ametambua maana ya kuwa na mwenzake wa kumsaidia katika ufanisi na pia kutafuta ushauri kutoka kwake.
"Natamani ningekuwa na mume ambaye anaweza angalau tu kunilipia gharama ya umeme, ama hata kuninunulia kemikali za dimbwi la kuogelea, ama hata bidhaa za jikoni yaani hata nyanya tuu," alisema Akothee.
Aliongeza kuwa maisha ya uhuni ni ngumu na kwamba ni wewe tu kutoka asubuhi hadi jioni, hakuna mtu wa kukupa ushauri, wa kukumbatia usiku au wa kukuamkua asubuhi.
"Nataka kuolewa na miaka 40 nimechelewa sana lakini nina imani," alisema Akothee.