Skip to main content

Utingo azua vituko kwa kusakata densi akikusanya nauli za abiria

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 18 June 2020.

Video iliyosambaa mitandaoni inaonyesha utingo huyo akisakata densi huku akikusanya nauli kutoka kwa abiria wake.

Utingo huyo kutoka Tanzania alijiwachilia hadharani wakati wimbo wa Diamond Platnumz ulianza kuchezwa.

Alianza kusakata densi safari ilipokuwa ikiendelea pindi tu wimbo wa Diamond Platnumz ulianza kuchezwa redioni.

Aliweka kazi yake kando na kuanza kuzikwenda huku abiria waliokuwa ndani ya gari hilo wakisalia kuangua kicheko wakifurahia walichokiona.

Video hiyo ilisambazwa katika ukurasa wa Instagram wa Wasafi TV ambapo wengi walitoa maoni yao wakielezea tamaa yao ya kukutana na utingo huyo.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →