Skip to main content

Mahakama Ya Nairobi Yashtaki Wakhungu na Waluke Kwa Kughushi KSh 297 Milioni

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 17 June 2020.

Wakhungu na Waluke Wanashtumiwa Kwa Kughushi KSh 297 Milioni

Mahakama ya Nairobi imetoa idhini ya kukamatwa kwa Grace Wakhungu, dada ya makamu wa rais wa zamani Moody Awori, na Mbunge wa Sirisia, John Waluke kwa kughushi kwa KSh 297 milioni.

Wakhungu na Waluke wanashtumiwa kwa kughushi kwa KSh 297 milioni, wakipokea pesa kupitia njia udanganyifu katika kandarasi kati yao na Chelsea Freight na Halmashauri ya Nafaka na Mazao (NCPB).

Kulingana na mashtaka iliyowasilishwa, Wakhungu na Waluke ni wakurugenzi wa Erad Suppliers Ltd, kampuni ambayo wanadaiwa kutumia kufuja KSh 297 milioni katika kandarasi hiyo.

Wawili hao wanashtumiwa kuwa mnamo Februari 24, 2009, wakiwa wakurugenzi wa kampuni hiyo, waliwasilisha stakabathi feki ya kuonyesha ushahidi ya tofauti zao na NCPB.

Hakimu Mwandamizi Elizabeth Juma alisema Wakhungu ambaye ana miaka 79, amekuwa akichezea mahakama mchezo wa paka na panya na kuchelewesha hukumu.

Wakili wa Wakhungu, Ian Wand aliambia mahakama kuwa mteja wake alilazwa mnamo Juni 7, katika Kituo cha Daima Afya Medical, mtaani Gumba na bado anaugua.

Hukumu itatolewa mnamo Juni 22.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →