Mkenya Hukamili Miaka Miwili Gerezani kwa Kuwalaghai Warwanda

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 18 September 2019.

September 17, 2019, gazeti la Rwanda la New Times liliripoti kwamba Victor Kinuthia, mmiliki wa kampuni ya Wealth Fitness, alipatikana na makosa ya kuwalaghai Warwanda na akapata kifungo cha miaka miwili gerezani.

Kinuthia alipanga mkutano wa utajiri mjini Kigali lakini ulitibuka baada ya mtafaruku kuhusu ada ya kuingia. Jaji alisema kulikuwa na ushahidi wa kuonyesha mkutano wa Kinuthia ulikuwa na nia ya kuwalaghai Warwanda.

Alisema mshukiwa alikuwa amewatumia Warwanda barua pepe ambapo alitumia taarifa za ujanja katika juhudi za kuwalaghai. Jaji huyo alikosoa Kinuthia na kusema hakuwa na ujuzi wowote wa kusaidia watu kutafuta utajiri.

Upande wa mashtaka uliambia mahakama kuwa Kinuthia alikuwa amewavutia Warwanda kwa kusema kuwa hakutakuwa na ada ya kuingia kwenye mkutano huo na watakaohudhuria watapata marupurupu fulani. Hilo halikufanya mbali baadaye watu walitakiwa kulipa ili kuhudhuria na kupata mafunzo.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...