Mbunge wa Makadara George Aladwa Amtetea Katibu wa Usalama wa Ndani Karanja Kibicho

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 16 September 2019.

Published on September 16, 2019, Mbunge wa Makadara George Aladwa amemtetea katibu wa Usalama wa Ndani Karanja Kibicho kuhusu madai kuwa anatumiwa kummaliza kisiasa Naibu Rais William Ruto.

Aladwa aliwataka viongozi wa Tangatanga kusita kumuingilia Karanja Kibicho, kwa sababu wana njama ya mambo fiche ambayo wanataka kutekeleza.

Aladwa alisema, "Nataka kumtetea Dr Kibicho na kuwaambia viongozi wawache kuhujumu kazi ya afiwa wa umma wakati ambapo anafanya kazi yake. Katibu huyo aliteuliwa na Rais Uhuru Kenyatta na anaifanya kazi ya rais," alisema Aladwa.

Aladwa alisema pia kwamba viongozi hao wamezoea siasa mbaya ya matusi, ukabila na kuwatenganisha watu hali ambayo BBI itashughulikia.

Aladwa alisema, "Viongozi hao wamezoea siasa mbaya ya matusi, ukabila na kuwatenganisha watu hali ambayo BBI itashughulikia, ndi kwa sababu hawajafurahia kwa sababu nchi inazidi kuungana," alisema Aladwa.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...