Picha za Moses Kuria zawasha moto kwenye mtandao

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 15 September 2019.

Mbunge wa Gatundu Kusini Moses Kuria alikuwa katika kipindi cha kujivinjari na viongozi wengine wakiwemo seneta wa Nairobi Johnson Sakaja na aliyekuwa mwenyekiti wa Jubilee David Murathe. Picha zao zilichapishwa huku zikizua hisia kali haswa baada ya kiatu cha binti kuonekana ndani ya chumba.

Wanamtandao waliteta viongozi wanajipa raha huku Wakenya wakiteseka. Kuria alikuwa pamoja na viongozi wengine wakiwemo seneta wa Nairobi Johnson Sakaja na aliyekuwa mwenyekiti wa Jubilee David Murathe.

Wanamtandao walichukua muda na kumlima Kuria [amoja na kikosi chake wakidao kuwa wanajivinjar wakati ambapo wananchi mashinani wanateseka. Hata hivyo, Kuria hakubabaika ila aliwatolea wafuasi wake picha nyingine huku akiwa ameshikilia kinywaji cha bei ghali aina ya Hennessy.

Wanamtandao walifanya upekuzi wao kiwango cha kujaribu kumfichua mmiliki wa kiatu hicho. Picha hii ya Moses Kuria iliibuka kwenye mtandao saa chache baada ya kuonekana kwenye nyingine wakiwa na vinywaji. Picha: Okor Ya'tan

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...