This archive report was first published on 13 September 2019.
Wakazi wa Nyandarua waliendelea na matumaini ya kumzika mwili wa Alice Njoki Njoroge Ijumaa, Septemba 13, mwili huo ulipowasili kwa ibada ya mazishi katika kijiji cha Olborosat kaunti ya Nyandarua.
Walipitia masaibu chungu nzima siku ambayo mwili huo uliondolewa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha JM Hospital huko Ol Kalou wakiwa na matumaini ya kumzika.
Barabara ilikuwa imeharibika kabisa na kusabaisha gari linaloendesha mwili huo kukwama katika matope kwa saa kadhaa.
Wakazi hao waliilaumu serikali ya kaunti kwa kutowajibika majukumu yake ya kukarabati barabara za eneo hilo.
Umoja ni nguvu. Jamaa na marafiki wa marehemu wamsaidia punda aliyekwama katika matope akiwa ameibeba maiti.