Murang'a: Kanisa Katoliki Kiharu Kuchukua Mkondo Mpya, Wanasiasa Wapigwa Marufuku

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 9 September 2019.

Maaskofu wa Kanisa Katoliki Kiharu, Kaunti ya Murang'a, wamepiga marufuku wanasiasa kushiriki katika shughuli za kanisa baada ya makonde yaliyovuma Jumapili, Septemba 8, 2019.

Uamuzi huo ulitolewa na Askofu James Wainaina, ambaye anasimamia kanisa zote eneo hilo.

Maaskofu hao wamepiga marufuku wanasiasa kwenye hafla zao kanisani, kwa kuwa wanasema kuwa tabia za Nyoro na 'babake' Kamanda ziliwasha shughuli za kanisa.

Utata ulitokea baada ya mbunge mteule Maina Kamanda kudinda Nyoro aongoze sherehe ya kanisa kwenye eneo bunge lake, akidai kuwa ni yeye alikuwa ameitwa kama mgeni wa heshima.

Wawili hao walionyesha ubabe wao na ghafla bin vuu ibada ikatibuka na kuwa uwanja wa cheche za siasa.

Maaskofu wamepiga marufuku wanasiasa kwenye kanisa katika kaunti hiyo, kwa kuwa wanasema kuwa tabia za Nyoro na 'babake' Kamanda ziliwasha shughuli za kanisa.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...