Barcelona Wanamtaka Lionel Messi Kusalia Klabuni Kwa Miaka Iliyosalia Ya Maisha Yake Ya Soka

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 9 September 2019.

Barcelona Wanamtaka Lionel Messi Kusalia Klabuni Kwa Miaka Iliyosalia Ya Maisha Yake Ya Soka

Mkataba wa sasa wa Lionel Messi na Barcelona unakaribia kutamatika katika muda wa miaka miwili, lakini Barcelona tayari wana mipango kuhusu hatma yake.

Kulingana na ripoti za SportsBible, Messi atakabithiwa mkataba mpya na Barcelona ambapo atakamilishia taaluma yake ya soka ugani Nou Camp.

Messi, mshindi huyo mara tano wa Ballon d'Or, amefunga mabao 419 katika mechi 452 za Barcelona, huku akijishindia mataji kadhaa katika kipindi cha miaka 15.

Kuanzia mwaka 2001, Messi alijiunga na Barcelona kupitia kijikaratasi cha nepi, na kuanza taaluma yake ya soka kama mchezaji wa Newell's Old Boys.

Viongozi wa Barcelona wanaamini kuwa Messi, ambaye bado anaendelea kupata nafuu, ni kifaa bora kwa Barcelona, na wanapania kuwa bado raia huyo wa Argentina, ataendelea kuwa na makali yake wakati wa mechi ya Kombe la Dunia la mwaka 2022, itakayoandaliwa nchini Qatar, ambapo atakuwa ametimu wa miaka 35.

Rais wa Barcelona Josep Maria Bartomeu anapania kutumia uhusiano wake na babake Messi, kupata saini yake wa mkataba mpya.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...