This archive report was first published on 8 September 2019.
Maandamano ya kisiasa yaliyotokea Jumapili, Septemba 8, 2019, katika kanisa Katoliki la Gatui, Kaunti ya Murang'a, ilikuwa ya kudumu. Kundi la Kieleweke, lililoongozwa na mbunge mteule Maina Kamanda, lilikuwa likishiriki ibada katika kanisa hilo.
Wakati huo huo, mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro, ambaye ni mmoja wa wafuasi sugu wa Naibu Rais William Ruto, alikuwa ameongoza kundi la Tangatanga katika kanisa hilo.
Maaskofu walibaki kinywa wazi baada ya wanasiasa hao kurushiana makonde mbele ya washirika. Inaarifiwa kwamba Nyoro na Kamanda walizozana baada ya kutofautiana kuhusu ni nani atawaalika viongozi kuzungumza.