Skip to main content

Shilingi Milioni 72 Zilizotupwa Kwa Kukosa Kwenye ATM Zinapatikana Msituni Kiambu

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 6 September 2019.

Polisi wamepata masanduku yaliyokuwa na shilingi milioni 72 zilizoibiwa kama yametupwa kwenye msitu Kaunti ya Kiambu.

Wakati huo huo, simu ya rununu pia ilipatikana katika eneo ambapo masanduku hayo yalikuwa yametupwa.

Polisi Kaunti ya Kiambu walisema masanduku hayo yalipatikana baada ya mkazi mmoja kuyaona na kufahamisha maafisa wa polisi.

Wafanyikazi wa kampuni ya G4S walikuwa wakizipeleka kwenye ATM za mabenki jijini Nairobi wakati waliokuwa wamevalia sare za polisi walitokea na kuwazubaisha kabla ya kutoweka na fedha hizo zote.

Wakenya kwenye mitandao walitaja wizi huo kama 'sinema kama vindio'.

Polisi wangali wanachunguza kisa hicho.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →