Skip to main content

Mwanamke Mwenye Matumaini: Pam Talbert Ateuliwa Naibu wa Mwalimu Mkuu Baada ya Kuhudumu kama Msafishaji

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 1 September 2019.

Mwanamke Mwenye Matumaini: Pam Talbert Ateuliwa Naibu wa Mwalimu Mkuu Baada ya Kuhudumu kama Msafishaji

Published on September 1, 2019

Pam Talbert, ambaye kwa wakati moja alikuwa akihudumu kama msafishaji shuleni, alikuwa mwenye bidii ya muchwa na mvumilivu ili kufikia kilele cha taaluma yake kama naibu wa mwalimu mkuu.

Alipokuwa na ulemavu wa kusoma, watoto wake walimsaidia kwenye ufanisi wake na kumlazimu kutoka kwenye starehe zake. Kila wanawe walipokuwa wakirejea kutoka shuleni, walikuwa wakimfunza mama yao.

Naibu huyo wa mwalimu mkuu mwenye bidii, alikuwa akijifunza kupitia kwa kile watoto wake walikuwa wakisoma shuleni. Hatimaye, aliweza kurejea shuleni na kufuzu na shahada ya mbili ikiwemo ya uzamili katika Chuo Kikuu cha Southern.

"Miujiza hufanyika kama unatafuta miujiza. Mimi ni miujiza. Sikuwa na uwezo wa kuandika wala kusoma. Nilikuwa katika darasa la tatu," alisema mama huyo.

"Licha ya kule unatoka, historia yako ama pale unaishi...mambo yatakuwa sawa endapo utavumilia ikiwa utajaribu," Talbert alisema.

Jambo la kufarahisha zaidi, Pam na mwanawe wa kiume wanapania kusomea shahada zao za uzamifu katika Chuo cha Southern University.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →