Gavana wa Machakos Alfred Mutua Azindua Kituo Cha Matibabu ya Saratani

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 29 August 2019.

Gavana wa Machakos Alfred Mutua Azindua Kituo Cha Matibabu ya Saratani

Kituo hicho kilizinduliwa mnamo Alhamisi, Agosti 29, 2019, katika hospitali ya Machakos Level V.

Kituo hicho kimejengwa na vifaa vya kisasa na kitaboresha matibabu ya wagonjwa wa saratani ambao watahudumiwa bila malipo.

Gavana wa Machakos Alfred Mutua alifichua kwamba, kituo hicho ambacho kimejengwa na vifaa vya kisasa kitaboresha matibabu ya wagonjwa wa saratani ambao watahudumiwa bila malipo.

Kituo hicho ambacho kimejengwa katika hospitali ya Machakos Level Five kilipokea ufadhili kutoka kwa wahisani mbali mbali ikiwemo Wizara ya Afya, taasisi ya kitaifa ya saratani, Path, Bioventures for Global Health, hospitali kuu ya Kenyatta, Ampath na Lions Club.

Wakazi wa Machakos ambao wamesajiliwa chini ya mwavuli wa Universal Health Coverage (UHC) watakuwa miongoni mwa wale ambao watapokea matibabu ya saratani bila malipo.

Kituo hicho pia kimejengwa ili kutoa ushauri nasaha kwa wagonjwa na familia zao.

Uzinduzi wa kituo hicho kumewapa matumaini Wakenya kwa jumla, kufuatia maafa ambayo yamesababishwa na saratani hususan kwa watu mashuhuri nchini.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...