This archive report was first published on 27 August 2019.
Wazee wa Kirinyaga wamewasilisha ombi mahakamani wakitaka kusajiliwa kama kabila la Akirinyaga na kutenganishwa na jamii ya Agikuyu.
Wazee hao wanaogopa kwamba lugha yao ina hatari ya kusahaulika ikiwa itaendelea kutegemea lugha ya Kikuyu.
Wizara ya Elimu imeziruhusu shule za msingi hususan za mashinani kuwatahini wanafunzi katika lugha za mama.
Wazee wa jamii ya Agikuyu wakati wa hafla ya hapo awali. Picha: Nation
Wazee wa Kirinyaga wanaogopa kwamba lugha yao ina hatari ya kusahaulika ikiwa itaendelea kutegemea lugha ya Kikuyu.
Wazee wa jamii ya Akirinyaga wakati wa hafla ya hapo awali. Picha: UGC
"Badala ya kuwafunza watoto wetu katika lugha ya Akirinyaga, wanafunzwa katika lugha ya Gikuyu. Iwapo hilo litaendelea watu wetu wa Akirinyaga hawatakuwepo tena siku za usoni," mmoja wa wazee hao alisema.