Skip to main content

Mwanga wa Kiswahili: Mazoea Mabaya Katika Kiswahili

N

Nyakundi Report

Newsroom 2 min read

This archive report was first published on 26 August 2019.

Makosa ya Mazoea Katika Kiswahili

Leo, tutakapofika, tutazidi kuangaza makosa ya mazoea katika matumizi ya lugha ya Kiswahili. Katika makala yetu ambayo yamepita, tumekuwa tukiweka mwanga katika Kiswahili na kuinyoosha lugha. Published on August 26, 2019

Leo, tutazidi kuona na kunyoosha palipo na utata. Picha: UGC

Makosa: Chakula Chenye Tulikula Kilikuwa Hakijaiva

Neno "chakula" limetumika visivyo. Sahihi: Chakula ambacho tulikula kilikuwa hakijaiva au Chakula tulichokula kilikuwa hakijaiva.

Makosa: Viongozi Wenye Tulichagua Ni Fisadi

Sahihi: Viongozi ambao tulichagua ni fisadi au Viongozi tuliowachagua ni fisadi.

Makosa: Gari Lenye Amenunua Ni Nzuri Sana

Sahihi: Gari ambalo amenunua ni zuri sana au Gari alililonunua ni zuri sana.

Makosa: Hakuna Binadamu Hapendi Maendeleo

Sahihi: Hakuna binadamu asiyependa maendeleo.

Makosa: Wanafunzi Wenye Walikalia Mtihani Mwaka Jana Walipasi Vizuri

Sahihi: Wanafunzi ambao walifanya mtihani mwaka jana walipasi vizuri au Wanafunzi waliofanya mtihani mwaka jana walipasi vizuri.

Makosa: Mtoto Yule Ni Mrefu Kuwaliko Wazazi Wake

Sahihi: Mtoto yule ni mrefu kuliko wazazi wake.

Makosa: Mtoto Yule Ni Mnene Kumliko Wake

Sahihi: Mtoto yule ni mnene kuliko wake.

Wakati unapotumia "o" rejeshi huwezi kutumia pamoja na kirejeshi amba. Mfano zaidi ya makosa haya ni;

Makosa: Mtu Ambaye Aliyekuja Alikuwa Mgeni Wetu

Sahihi: Mtu ambaye alikuja alikuwa mgeni wetu au Mtu aliyekuja alikuwa mgeni wetu.

Kumbuka Kiswahili ndio fimbo ya Mwafrika tuitumie.

Makala haya yameandikwa na Sakwa Titus mwalimu, mhakiki na mwandishi.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →