This archive report was first published on 22 August 2019.
Mwanawe wa Mwanamuziki Bahati Aondolewa Hospitalini kama Mfalme na Magari ya Kifahari ¶
Mnamo siku ya Jumatano, Agosti 14, 2019, mtandao ulikuwa umewaka moto kufuatia kuzaliwa kwa mwanawe wa kiume wa mwanamuziki wa nyimbo za Injili, Majesty Bahati.
Baada ya kuwa hospitalini kwa wiki moja, malaika huyo hatimaye amepelekwa nyumbani, ambapo alionekana kukaribishwa duniani kama mfalme.
Alipewa shupavu wakati wa kipindi chote akiwa mjamzito na pia wakati wa kujifungua, na baba huyo wa watoto wanne alitoa picha ya uso wa mwanwe bila kusudia kwenye mtandao jamii.
Shabiki wa Bahati walikuwa wamejitokeza kwa wingi kupata fursa ya kuona sura ya mtoto huyo, na Diana Marua, mkewe, alikuwa akionekana kuwa mchovu lakini uso wake ulikuwa umejawa na furaha akitazama mapenzi ambayo mtoto wake wa wiki moja alionyeshwa muda mfupi tu baada ya kuzaliwa.