This archive report was first published on 20 August 2019.
Msichana wa Chuo Kikuu Lilian Faye, ambaye anasoma uanasheria Chuo Kikuu cha Nairobi, alisimulia masaibu yake ya kumea ndevu katika tukio lililotokea mwaka 2019.
Alisema alijipa moyo kwa sababu hata mamake alikuwa na kindevu kimoja, lakini siku moja maji yalizidi unga wakati ambapo mwanafunzi mwenzake alimfanyia utani kutokana na ndevu zake.
"Siku moja shuleni, rafiki yangu akaniambia Faye unamea ndevu," alisema.
"Nikacheka na kusema labda tu mimi ni tofauti na wengine," aliongeza.
Alipitia mengi huku watu wakishangaa ni vipi binti mwenye urembo kama kama wake alikuwa akimea ndevu.
Alisema alijipata pabaya zaidi baada yake kupata sauti nzito kama vile wanaume.
Alisema alijipata pabaya zaidi baada yake kupata sauti nzito kama vile wanaume.
"Kwa kweli sikuchagua kumea ndevu lakini natumai watu watawacha kuwaona kama watu tofauti. Si kupenda kwetu, kwa hivyo wanawake waote ambao wako na ndevu hapo nje, nyinyi ni warembo," alisema.