Skip to main content

Raila's 2022 Presidential Ambitions Spark Debate

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 20 August 2019.

Uchaguzi wa urais wa 2022 unakuja kwa haraka, na Raila Odinga anaibuka kama mmoja wa wapinzani wa kwanza. Mbunge wa Westlands Tim Wanyonyi amesema Raila atakuwa kwenye debe kwenye kinyang'anyiro cha urais na ndiye yuko na nafasi bora zaidi kuibuka mshindi.

Wanyonyi alisema Raila ameweka mikakati kabambe ili kuhakikisha anaibuka mshindi katika uchaguzi wa urais wa 2022. Akiongea katika kanisa moja huko Kayole Jumapili, Agosti 18, Wanyonyi alisema Raila ameweka mikakati kabambe ili kuhakikisha anaibuka mshindi.

"Kwa wale wanaoshuku ama kujiuliza iwapo atakuwepo, nataka niwaeleze kuwa Raila Odinga atakuwa kwenye debe la urais 2022 na ndiye ambaye atakuwa rais wetu," Wanyonyi alisema.

Wanyonyi aliongeza kuwa yuko katika mstari wa kwanza kupigia debe handshake kati ya Raila na Rais Uhuru Kenyatta. Aliongeza kuwa handshake itawezesha kuwe na mageuzi ya kikatiba ili kutengeneza nyadhifa zaidi.

Kituo kimoja cha habari humu nchini kinafaa kukoma kuzungumza kwa niaba ya Raila baada ya alitangaza atawania urais 2022. Katibu wa ODM Edwin Sifuna vile vile alisema kuwa vyombo vya habari vinafaa kukoma kuzungumza kwa niaba ya mdosi wake.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →