Raila's 2022 Presidential Ambitions Spark Debate

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 20 August 2019.

Uchaguzi wa urais wa 2022 unakuja kwa haraka, na Raila Odinga anaibuka kama mmoja wa wapinzani wa kwanza. Mbunge wa Westlands Tim Wanyonyi amesema Raila atakuwa kwenye debe kwenye kinyang'anyiro cha urais na ndiye yuko na nafasi bora zaidi kuibuka mshindi.

Wanyonyi alisema Raila ameweka mikakati kabambe ili kuhakikisha anaibuka mshindi katika uchaguzi wa urais wa 2022. Akiongea katika kanisa moja huko Kayole Jumapili, Agosti 18, Wanyonyi alisema Raila ameweka mikakati kabambe ili kuhakikisha anaibuka mshindi.

"Kwa wale wanaoshuku ama kujiuliza iwapo atakuwepo, nataka niwaeleze kuwa Raila Odinga atakuwa kwenye debe la urais 2022 na ndiye ambaye atakuwa rais wetu," Wanyonyi alisema.

Wanyonyi aliongeza kuwa yuko katika mstari wa kwanza kupigia debe handshake kati ya Raila na Rais Uhuru Kenyatta. Aliongeza kuwa handshake itawezesha kuwe na mageuzi ya kikatiba ili kutengeneza nyadhifa zaidi.

Kituo kimoja cha habari humu nchini kinafaa kukoma kuzungumza kwa niaba ya Raila baada ya alitangaza atawania urais 2022. Katibu wa ODM Edwin Sifuna vile vile alisema kuwa vyombo vya habari vinafaa kukoma kuzungumza kwa niaba ya mdosi wake.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...