Michael Olunga aifungia Kashiwa Reysol bao la ushindi nchini Japan

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 18 August 2019.

Michael Olunga, mvamizi wa timu ya Kashiwa Reysol, amefunga mabao 12 katika Ligi Kuu ya Japan, J2, nyuma ya Lee Yong-Jae ambaye anaongoza kwenye orodha hiyo.

Olunga alifunga mabao matatu kwa mpigo siku chache zilizopita, na kufanya kazi kwa pamoja na timu yake ili kushinda V-Varen Nagasaki 2-1 mnamo Jumamosi, Agosti 17.

Mechi ilianza kwa Reysol kupata ushindi wa mapema kupitia kwa mkwaju kutoka kwa Matheus Savio, ambaye aliweka wageni hao kifua mbele kunako dakika ya nane ya mchezo.

Wenyeji walisawazisha bao hilo baada ya dakika tano kabla ya kipindi cha pili, huku Hiroto Goya akivurumisha kombora lake lililotuwa nyumbani kimyani.

Olunga alitoa bao lake la ufundi na kukisaidia kikosi chake kushikilia ushindi wao wa kwanza na kujipatia pointi nyingine wakiwa ugenini.

Ushindi huo ulifungua mwanya wa mkubwa wa pointi saba ya Reysol ambao ni wa kwanza kwenye jedwali kwa pointi 58.

Olunga amefunga mabao 12, huku zikiwa ni tofauti ya mabao matano ya Lee Yong-Jae, ambaye anaongoza kwenye chati ya watingaji bora wa mabao.

Atakuwa na kibarua cha kumbwaga Lee kwenye nafasi hiyo wakati timu yake itakutana na Gifu katika mechi yao nyingine.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...