This archive report was first published on 13 August 2019.
Kiteta, Mbooni, Kenya - Mwanamke alimtoka nyumbani baada ya kumvunja vyombo vyake akiwa mlevi. Hii ilikuwa baada ya kalameni alivyokuwa akiinywa pombe kupindukia na aliishi kumpuuza mkewe kila apokuwa akimuonya dhidi ya tabia yake.
Alipofika nyumbani, jamaa alifika chakari na kufululiza hadi jikoni. Kwa bahati mbaya, akiwa huko, aliangukia meza iliyokuwa na vikombe na sahani na kuvivunja nyote.
Alipovunja vyombo, mama alikuwa na ujumbe wa kutosha. "Yaani, umeleta ulevi jikoni. Ona sasa matokeo ya ulevi. Kwa nini unavunja vyombo vyangu? Nilikuambia uache pombe lakini ukakataa. Leo sitavumilia. Umenitesa kwa muda mrefu. Pombe utaacha," mama aliwaka huku akisanya vyake na kuondoka.
Penyenye zinaarifu kwamba, mama hakumpa kalameni nafasi ya kujitetea. Kalameni aliachwa mataani huku akigubikwa na machozi akijutia tabia yake.
Published on August 13, 2019 by Tuko.