Sponsa 'Kumla' ataka Aolewe na Mwanawe: Drama ya Kipusa wa Thika

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 9 August 2019.

Kituo cha Habari cha Taifa Leo kinatoa taarifa kwamba mwanadada alijikuta pabaya na kuanza kububujikwa baada ya shuga daddy wake kumtaka aolewe na mwanawe.

Demu na sponsa walikuwa wameishi pamoja kwa muda mrefu, na mwanadada alikuwa akitaka amuoe.

Alidai kwamba tayari alikuwa ana familia yake, na kwa hivyo, hakuwezi kukuoa mwanadada.

"Mimi siwezi kukuoa kwa sababu tayari nina mke na watoto. Ningependa uolewe na mwanangu na nitagharamia kila kitu. Nitakuwa nikikufanyia kila kitu," buda alimwambia mrembo.

Demu alichukizwa na kauli ya buda na akaanza kumkaripia huku akidai kwamba hilo halingewezekana.

"Wewe ni mtu wa sampuli gani? Nimekuwa mpenzi wako kwa muda mrefu na sasa unataka niolewe na mwanao. Una akili timamu wewe? Haiwezekani na haitawezekana," kipusa aliapa huku akitishia kumsema jamaa kwa mkewe na jamii yake nzima.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...