Mwanamke Achoshwa na Upweke, Azua Kioja Kupiga Mayowe Mjini Akimsaka Mume

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 8 August 2019.

Mwanamke Achoshwa na Upweke, Azua Kioja Kupiga Mayowe Mjini Akimsaka Mume

Video iliyosambaa Twitter inaonyesha mwanamke huyo akizunguka mjini akiwaamsha watu waliokuwa wamelala huku akipiga mayowe.

Alisimama katika eneo la kuegesha magari na kuwaarifu watu wote waliokuwepo eneo hilo alikuwa amezidiwa na upweke na kwamba alikuwa akimsaka mchumba.

"Amkeni! Namsaka mchumba! Nina upweke mimi! Nimesimama hapa nje," alisema.

Video hiyo ilisambazwa Twitter huku wengi wakiachwa vinywa wazi na jinsi mwanamke huyo aliyoonesha ujasiri wa kuzua kioja hicho.

Wengi wamekataa kusema kwamba mwanamke huyo alikuwa akijitafutia umaarufu, huku wengine wakihisi kwamba jamii imechangia mambo kama hayo kwa kuwashinikiza watu kutafuta wachumba na kuolewa.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...