Mwanariadha atiwa mbaroni kuhusiana na kifo cha mwalimu wa shule ya upili

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 8 August 2019.

Maafisa wa polisi mjini Eldoret wamemtia mbaroni mwanariadha anayecheza Marekani kufatia kifo cha mwalimu wa shule ya upili katika mtaa wa Outspan.

Alama ya kifo ya Gloria Sangutei ilipatikana Jumatatu, Agosti 5, karibu na shamba la mahindi, na mwili huo ulikuwa na alama za kifo.

Polisi walisema mshukiwa, anayedaiwa kuwa mume wa marehemu, alikamatwa na kuzuiliwa baada ya kujisalimisha polisi Jumanne, Agosti 6.

Francis Warui, Kamanda wa Polisi wa Kaunti ndogo ya Kapseret, alisema mshukiwa alijitokeza katika Kituo cha Polisi cha Kiambaa akitaka kufahamu ikiwa ni mke wake aliyekuwa amepatikana ameuawa katika shamba la Ancilla, Outspan.

Warui alisema, "Mshukiwa alijitokeza katika Kituo cha Polisi cha Kiambaa akitaka kufahamu ikiwa ni mke wake aliyekuwa amepatikana ameuawa katika shamba la Ancilla, Outspan. Lakini alitoa taarifa kinzani alipohojiwa na polisi Langas,".

Warui aliongeza, "Tutamhoji kuhusiana na tukio hilo. Tukipata hakuna uhusiano unaomtia hatiai, ataachiliwa huru."

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...