Mtoto wa miaka 7 wa India alikuwa na meno 526 kwenye ufizi wake

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 2 August 2019.

Mtoto wa miaka 7 wa India alikuwa na shida kubwa kwa sababu ya meno 526 kwenye ufizi wake, kulingana na taarifa kutoka kwa madaktari waliofanyia upasuaji.

Mtoto huyo alikuwa amelazwa hospitalini mwezi Julai baada ya kudai alikuwa akihisi maumivu kwenye ufizi wake wa chini.

Madaktari walimfanyia skana na walichopata kiliweza kuwaduwaza kwani mtoto huyo kando na meno 32 alikuwa na meno mengine 526.

Uvimbe huo kwa jina odontoma, ulikuwa ukitatiza meno yake kutomea kama kawaida.

Punde uvimbe huo ulipogunduliwa, madaktari hao walichukua hatua ya haraka ya kumfanyia upasuaji na kutoa meno hayo kwenye ufizi wake wa chini.

Odontoma ni uvimbe ambao hauwezi kusababisha saratani na pia ni aina ya magojwa ya meno ya hamartoma.

Hamartoma ni hali ambayo seli tofauti hukutana na kuanza kuoata katika sehemu fulani ya mwili hususan ufizi wa chini.

Mmoja wa madaktari aliyemfanyia mtoto huyo upasuaji alisema, "Kulikuwa na jumla ya meno 526 kuanzia milimita 0.1 (inchi 0.4) hadi milimita 15 (inchi 0.6). Kipande kidogo pia kilikuwa na mizizi ya kuonyesha ilikuwa jino."

Mvulana huyo aliondoka hospitalini baada ya kulazwa kwa siku tatu na anatazamiwa kupona.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...