This archive report was first published on 2 August 2019.
Alhamisi Agosti 1, mwakilishi wa familia ya Mbunge wa Kibra Ken Okoth alikubaliana na familia ya Anne Muthoni Thumbi kuhusu DNA na kuteketeza mwili wa marehemu.
Thumbi alikwenda kortini na kufanikiwa kusimamisha mazishi ya Okoth baada ya kudai familia ya marehemu ilikuwa imekataa kumtambua mtoto wake kuwa mtoto wa mwenda zake.
Uchunguzi wa DNA utafanywa ili kubaini ukweli kuhusu madai ya Thumbi huku mwili wa marehemu Okoth utateketezwa Jumamosi Agosti 3.
Thumbi alijitokeza na kutaka yeye na mwanawe wa kiume kuhusishwa katika programu ya mazishi ya marehemu.
Ukubaliano huu ni matokeo ya makubaliano ya pili kati ya pande zote mbili.