Takriban Wabunge 60 wanaugua Saratani, Gavana Sonko anasema

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 29 July 2019.

Gavana wa Nairobi Mike Sonko amesema kuwa takriban wabunge 60 wanaugua saratani, kwa mujibu wa ripoti zake.

Alisema hii wakati wa kuomboleza mbunge Joyce Laboso ambaye alifariki dunia Jumatatu, Julai 29, baada ya kuugua saratani.

Laboso alikuwa Gavana wa Kaunti ya Bomet.

Alisema ugonjwa huo sasa ni jinamizi na serikali inafaa itafute mbinu za kukabili.

Alisema hii wakati wa kuwataka viongozi wajitokeze ili waweke mikakati ya jinsi ambavyo watapigana na janga hilo.

"Saratani ni ungonjwa ambao unakithiri sana, ripoti ambazo tunapata ni kuwa kuna wabunge sitini ambao wanaugua ugonjwa huu wa saratani na lazima tuketi chini kama viongozi na tupange jinsi tutakabiliana nao," Mike Sonko alisema.

Wabunge wengine wanaugua saratani ni Francis Waititu, ambaye alisema aliweza kupokea matibabu na kwa sasa ana nafuu ya kutosha kuchapa kazi.

Waititu alisema, "Watu wengi sana wanaugua Saratani. Hakuna mtu anataka kuongea kutokana na unyanyapaa unaohusishwa na saratani. Nchini India, nilikutana na mamia ya wanaougua saratani kutoka Kenya," Mbunge huyo alisema.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...