This archive report was first published on 27 July 2019.
Benard Shinali, mbunge wa Ikolomani, amefariki Marekani, Ijumaa, Julai 26, 2019, akiwa na umri wa miaka 35.
Alifariki akiwa katika kidimbwi cha kuongelea katika eneo la Arizona, huku familia yake ikijaribu kumuokoa mtoto.
Robert Ayisi, ndunguye wa Shinali na msemaji wa familia, alisema kwamba familia hiyo ilipokea taarifa ya kifo cha mwanao kutoka kwa jamaa yake ambaye alihudumu pamoja na Shinali katika jeshi.
"Tulipokea habari ya kuhusu kifo chake kutoka kwa jamaa wake ambaye wanahudumu pamoja katika jeshi. Masaka anaishi katika eneo la Illinois ila alisafiri Arizona kwa likizo na familia yake kabla ya kifo chake," Ayisi alisema.
Wabunge kadhaa kutoka kaunti ya Kakamega, ikiwemo seneta Cleophas Malala na mbunge wa Navakholo Emmanuel Wangwe, walizuru makazi ya mbunge huyo ili kutoa pole zao kwake.
Marehemu amemwacha mjane na watoto wawili.