Gavana Waititu na Mkewe Wakamatwa Baada ya DPP Kuagiza

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 27 July 2019.

Gavana Waititu na Mkewe Wakamatwa Baada ya DPP Kuagiza

Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) Noordin Haji ameamuru kukamatwa Gavana wa Kiambu Ferdinand Waititu na mkewe Susan Wangari kwa ubadhirifu wa KSh 588 milioni.

Wakati wa kukamatwa, Waititu anaweza kushutumiwa na mashtaka ya matumizi mabaya ya mamlaka.

Maafisa wa Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC) walivamia makazi ya Waititu mapema asubuhi Jumamosi, Julai 27, lakini hawakuwakuta nyumbani.

Maafisa hao walikamatwa washukiwa wengine watatu kwenye sakata inayohusisha KSh 588 milioni.

Washukiwa hao ni Mkurugenzi wa M/s Testimony Enterprises Limited Charles Mbuthia Chege, mwanachama wa kamati ya masuala ya ununuzi Joyce Ngina Musyoka na Simon Kabocho Kangethe.

Waititu anadaiwa kupeana zabuni ya thamani ya KSh 588, 198, 328 bila ya kufuata utaratibu unaofaa, pesa zilizokuwa zimetegewa ujenzi wa barabara kadhaa Kiambu katika mwaka wa fedha wa 2017/2018.

Sehemu ya pesa hizo zilitumika na Saika Two Estate Developers kununua Hoteli ya Bienventure Delta inayomilikiwa na gavana huyo na mkewe.

Waititu ameorodheshwa kuwa mmoja wa wamiliki wa Saika Two Estate Developers.

Maafisa wa EACC wameeleza kuwa Waititu na mkewe wamejificha baada ya kuamuru kukamatwa kwao.

Maafisa hao wameeleza kuwa hajaonekana tangu Ijumaa usiku hata baada ya maafisa kuzuru maboma yake wakimtafuta.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...