This archive report was first published on 26 July 2019.
Kituo cha habari Tuko.co.ke liliripoti kuwa mwanamke wa Tunduimuni alijikuta mashakani baada ya mkewe kufunganya virago na kurejea kwao baada ya mumewe kumuuza mbuzi wake.
Penyenye zinaarifu kwamba mwanamke huyo alichukizwa na kuapa kutorejea katika ndoa hiyo na kushi na mume ambaye alisema hana bidii ya kutafuta mali.
Alipokuwa ameenda kuhudhuria mafunzo ya ukulima kwa muda wa siku tatu, mama huyo alipigwa na butwa kupata mbuzi wake hawapo.
Alikusanya kila kitu alichokuwa amenunua chumbani mwao na kurejea kwa wazazi wake.
Alisema kuwa ana bidii kama ya mchwa, lakini mumewe amezongwa na ulevi kazi ni kubugia tu.